Matokeo ya Darasa la Saba 2022 - 2023

  psle-2022 examination results - NECTA https://matokeo.necta.go.tz  › psle2022 › psle

Jumatano, 22 Novemba 2017

MAJINA YA VINASABA

Majina ya nasaba
Nasaba
Nasaba ni uhusiano wa kizazi baina ya watu. Uhusiano huu unaweza kuwa katika familia au ukoo mmoja au uzao mmoja.
1. Mama/nina: Mzazi wa kike.
2. Baba: Mzazi wa kiume.
3. Kaka: Ndugu wa kiume.
4. Dada: Ndugu wa kike.
5. Nyanya/Bibi: Mama/Mzazi wa kike wa baba au mama.
6. Babu: Baba/Mzazi wa kiume  wa mama au baba.
7. Mjukuu: Mtoto wa mwana.
8. Kitukuu: Mwana wa mjukuu.
9. Kilembwe: Mwana wa kitukuu.
10. Kilembwekeza/kining’ina: Mwana wa kilembwe.
11. Kitojo : mtoto wa kilembwekeza.
12. Ami/amu: Kaka wa baba.
13. Shangazi: Dada wa baba.
14. Mjomba/hau: Kaka wa mama.
15. Halati/hale: Dada wa mama.
16. Mkazahau/Mkazamjomba: Mke wa mjomba.
17. Mkazamwana: Mke wa mwana.
18. Mavyaa: Mama wa mume.
19. Bavyaa: Baba wa mume.
20. Mamamkwe: Mama wa mke.
21. Babamkwe: Baba wa mke.
22. Mcheja: Baba au mama wa mke au mume (mkwe).
23. Kivyere : Jina linalotumika kuitana wazazi wa mke na wazazi wa mume
24. Mpwa: Mtoto wa dada wa mtu mwanamume, jina analotumia mjomba kumwita mtoto wa dada yake.
25. Mkoi: Mtoto wa shangazi au mjomba
26. Binamu: Mwana wa kiume wa ami (ami/amu ni Ndugu wa kiume wa baba.)
27. Bintiamu: Mwana wa kike wa ami.
28. Shemeji: Ndugu wa mke au ndugu wa mume. Pia ni Rafiki wa kiume wa mume au rafiki wa kike wa mke.
29. Mama wa kambo: Mama asiyekuzaa lakini anakulea.
30. Baba wa kambo: Baba asiyekuzaa
31. Umbu: Jina waitanalo kaka na dada.
32. Ndugu mlungizi: Ndugu anayekufuata nyuma. (mdogo wako anayekufuata)
33. Wifi:
(a) Mke wa kaka. Iwapo wewe ni msichana, mke wa kaka yako utamwita wifi.
(b) Dada wa mume: Iwapo msichana ameolewa dada wa mumewe atamwita wifi.
34. Mwamu/mlamu:
a) Kaka wa mke. Mwanamume akioa, kaka wa mkewe atamwita mlamu.
b) Mume wa dada: mvulana au mwanamume atamwita mume wa dadaye – mlamu.
35. Mwanyumba: Wanaume waliooa katika familia moja.
36. Mkemwenza/mitara: Jina wanalotumia wanawake walioolewa na mwanamume mmoja.
37. Kifungamimba/ kitindamimba/ mzuwanda: Mtoto wa mwisho kuzali- wa katika familia.
38.Mwanambee/kifunguamimba/kichinjamimba: Mtoto wa kwanza kuzaliwa katika familia.
39. Nyanyamkuu: Mama wa nyanya.
40. Babu mkuu: Baba wa babu.
41. Maharimu: Mtu usiyeweza kumwoa au kuolewa naye kwa sababu ya uhusiano wa nasaba.
42. Mnuna: Ndugu ndugu mdogo.

s.kitaly86@gmail.com