WIZARA YA ELIMU, SAYANSI,
TEKNOLOJIA NA UFUNDI
SHULE YA SEKONDARI MWINUKO
MTIHANI WA NUSU MHULA WA KWANZA MACHI 2018
KISWAHILI KIDATO CHA PILI.
Muda: SAA 2:00 Jumanne,
20 Machi 2018 mchana
Maelekezo
i. Karatasi hii ina
sehemu A, B, C, D na E
ii. Jibu masali yote.
iii. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa.
SEHEMU A. (ALAMA 15)
UFAHAMU
i. Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali
yanayofuata.
Kati ya lugha rasmi za jamii fulani moja inaweza kuteuliwa
kuwa ni ya taifa. Kwa desturi, mbali na kutambuliwa kwa matumizi ya aina
mbalimbali lugha ya taifa huwa ni kitambulisho cha taifa.
Mathalani kitu kinachomtambulisha Mngoni ni Kingoni chake.
Hivyo basi kitambulisho cha
kwanza cha mtu wa taifa fulani ni Lugha ya taifa hilo. Kwa jinsi hii, lugha ya
taifa huakisi na kuchukua utamaduni wa taifa. Hivi ni kusema kwamba lugha ya
taifa, hueleza ufasili wa
taifa, kujenga umoja pamoja na kuwafanya watu wataifa hilo wajihisi kuwa
wamoja.
Ingawa lugha rasmi inaweza kuwa lugha ya kigeni,haitokani na
kundi lolote kati ya makundi yanayoikamilisha. Lakini lugha ya taifa mara
nyingi huwa na mizizi ndani ya taifa lenyewe au huwa ni lugha inayozungumzwa na
watu ndani ya nchi hiyo.
Kwa mfano ni muhali
kisikia nchi moja ya Kiafrika kutangaza Kireno au Kiingereza kuwa lugha ya
taifa. Linaloyamkinika hapa ni kuwa na mataifa yaliyotawaliwa na Wareno
yatalazimika walau kwa miaka ya mwanzo kukitambua Kireno kuwa miongoni mwa
lugha rasmi za taifa jipya.
Miongoni mwa sababu zinazofanya mataifa kuteua lugha ya
asili kuwa lugha ya taifa lenyewe ni kwamba lugha hiyo haina budi kuwa
inatumiwa na watu wengi na inaweza kufundishika kwa urahisi.
MASWALI
i. Pendekeza kichwa
kifaacho kwa habari hii. ……………………………………………………
ii. Kwa mujibu wa habari hii lugha ya taifa
hupatikanaje?………………………
iii. Bainisha sifa nne za lugha ya taifa
iv. Taja dhima tatu za lugha.
v. Nini maana ya maneno yaliyokolezwa wino kwa mujibu wa habari
uliyoisoma?
a. Kitambulisho ………………………………………………………………………
b. Ufasili
……………………………………………………………………………….
c. Muhali
……………………………………………………………………………...
SEHEMU B. (ALAMA 15)
MATUMIZI YA LUGHA NA USAHIHI
WA MAANDISHI
2. A. Taja na fafanua kwa mifano mambo makuu manne ambayo
mzungumzaji huzingatia katika kuteua maneno na miundo ya tungo zake. (alama 05)
B. Onesha mazingira ambamo lugha ya tungo
zifuatazo hutumika. (alama 05)
i.
Yesu anakupenda anataka akuokoe
………………………………………………….
ii.
Chapa hizi barua haraka haraka
……………………………………………………..
iii.
Nani chai ……………………………………………………………………………..
iv.
Kaza msuli baba, nyanyua zigo, twende
juu………………………………………….
v.
Nipimie unga kilo
tano………………………………………………………………..
C. Sahihisha makosa katika sentensi zifuatazo
kwa kuziandika kwa usahihi. (alama 05)
i.
Ninachukua
nafasi hii kuwashukuru
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
ii.
Weka sahihi yako
hapa.
Kosa:
……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
iii.
Sikuwa najua
kuwa mwalimu wa Kiswahili anaitwa Mshiu.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
iv.
Katika ajali
hiyo watu kumi waliuwawa.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
v.
Ninakwenda kesho
kwa mjomba.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
SEHEMU C. (ALAMA 15)
SARUFI
3. A. Eleza waziwazi kuhusu kazi za viambishi
vilivyopigiwa mstari katika maneno yafuatayo. (alama 06)
(a)
A-nacheza (kazi mbili)
(b)
Ana-vi-penda (kazi mbili)
(c)
Ruk-a (kazi moja)
(d) Ana-ye-fundisha
(kazi moja)
B. Kupitia
taaluma ya unyambulishaji badili majina/Nomino zifuatazo-kuwa vielezi (alama
03)
i.
Nyumba ……………………………………………………………………............
ii.
Bustani …………………………………………………………………….............
iii.
Hewa ……………………………………………………………………................
iv.
Daraja ……………………………………………………………………...............
v.
Kitanda . …………………………………………………………………….............
vi.
Uwanja ………………………………………………………………………………..
C. Chunguza
jedwali lifuatalo kwa makini kasha jaza sehemu zilizoachwa wazi. ( alama06)
|
Neno
|
Mzizi
|
Kauli ya Kutendana
|
Kauli ya Kutendwa
|
|
Kusema
………………
Kuomba
………………
……………….
|
……………. …………….
…………….
-andik-
…………….
|
…………………..
Kupigana
Kuombana
…………………..
Kuimbana
|
Kusemwa
…………………….
…………………….
Kuandikwa
……………. ………
|
SEHEMU D. (ALAMA 40)
FASIHI SIMULIZI
4. A. Kazi za fasihi simulizi zina umuhimu gani kwa jamii? (alama 10)
B. Kamilisha methali zifuatazo. (alama 10)
i.
………………………………………..……………
yasiyo na ncha.
ii. Usidharau dafu …………………………….……………………….
iii. …………………………………….…………si mwisho wa uhunzi.
iv. ………………………………………………………… i maji.
v. Mtumi wa kunga ……………………………..…………………
D. Eleza kwa ufupi maana ya dhana zifuatazo
kwa kutumia mifano halisi. (alama 20)
i. Ubeti
ii. Kipande
iii. Mizan
iv. Urari
v. Vina
SEHEMU E. ( ALAMA 15)
UANDISHI WA INSHA/UTUNGAJI
5. A. Mtumie
simu ya maandishi baba yako aitwaye Michael Martin wa Sanduku la Posta 333
Moshi, ukiweleza kuhusu mdogo wako aitwaye Maringo Michael aliyevunjika mguu
wakati akicheza mpira wa miguu katika mashindano ya UMISETA yaliyofanyika
katika uwanja wa Shule ya Bwiru Wavulana. Jina lako ni Shukuru Michael. (simu yako iwe na maneno kumi tu ) (alama
05).
B. Chora kielelezo cha muundo wa Barua Rasmi.
(alama 10)
------------------------------- MWISHO ------------------------------------
Jua na Mwezi Havifanyi Kazi
kwa Pamoja Japo Vyote Hutoa Mwanga.
*******************************************************************************************
† † † † † MR. MSHIU S.E † † † † †
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni