Matokeo ya Darasa la Saba 2022 - 2023

  psle-2022 examination results - NECTA https://matokeo.necta.go.tz  › psle2022 › psle

Jumapili, 1 Aprili 2018

Mtihani wa Kiswahili Kidato cha pili

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI
SHULE YA SEKONDARI MWINUKO
 MTIHANI WA NUSU MHULA WA KWANZA MACHI 2018

KISWAHILI KIDATO CHA PILI.

Muda: SAA 2:00                                                                   Jumanne, 20 Machi 2018 mchana
Maelekezo
i. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E
ii. Jibu masali yote.
iii. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa.

SEHEMU A. (ALAMA 15)
UFAHAMU
i. Soma kwa makini habari ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata.
Kati ya lugha rasmi za jamii fulani moja inaweza kuteuliwa kuwa ni ya taifa. Kwa desturi, mbali na kutambuliwa kwa matumizi ya aina mbalimbali lugha ya taifa huwa ni kitambulisho cha taifa.
Mathalani kitu kinachomtambulisha Mngoni ni Kingoni chake. Hivyo basi kitambulisho cha kwanza cha mtu wa taifa fulani ni Lugha ya taifa hilo. Kwa jinsi hii, lugha ya taifa huakisi na kuchukua utamaduni wa taifa. Hivi ni kusema kwamba lugha ya taifa, hueleza ufasili wa taifa, kujenga umoja pamoja na kuwafanya watu wataifa hilo wajihisi kuwa wamoja.
Ingawa lugha rasmi inaweza kuwa lugha ya kigeni,haitokani na kundi lolote kati ya makundi yanayoikamilisha. Lakini lugha ya taifa mara nyingi huwa na mizizi ndani ya taifa lenyewe au huwa ni lugha inayozungumzwa na watu ndani ya nchi hiyo.
Kwa mfano ni muhali kisikia nchi moja ya Kiafrika kutangaza Kireno au Kiingereza kuwa lugha ya taifa. Linaloyamkinika hapa ni kuwa na mataifa yaliyotawaliwa na Wareno yatalazimika walau kwa miaka ya mwanzo kukitambua Kireno kuwa miongoni mwa lugha rasmi za taifa jipya.
Miongoni mwa sababu zinazofanya mataifa kuteua lugha ya asili kuwa lugha ya taifa lenyewe ni kwamba lugha hiyo haina budi kuwa inatumiwa na watu wengi na inaweza kufundishika kwa urahisi.
MASWALI
i. Pendekeza kichwa kifaacho kwa habari hii. ……………………………………………………
ii. Kwa mujibu wa habari hii lugha ya taifa hupatikanaje?………………………
iii. Bainisha sifa nne za lugha ya taifa
iv. Taja dhima tatu za lugha.
v. Nini maana ya maneno yaliyokolezwa wino kwa mujibu wa habari uliyoisoma?
a.      Kitambulisho ………………………………………………………………………
b.      Ufasili ……………………………………………………………………………….
c.      Muhali ……………………………………………………………………………...

SEHEMU B. (ALAMA 15)
MATUMIZI YA LUGHA NA USAHIHI WA MAANDISHI
2. A. Taja na fafanua kwa mifano mambo makuu manne ambayo mzungumzaji huzingatia katika kuteua maneno na miundo ya tungo zake. (alama 05)

   B. Onesha mazingira ambamo lugha ya tungo zifuatazo hutumika. (alama 05)
i.        Yesu anakupenda anataka akuokoe ………………………………………………….
ii.      Chapa hizi barua haraka haraka ……………………………………………………..
iii.    Nani chai ……………………………………………………………………………..
iv.    Kaza msuli baba, nyanyua zigo, twende juu………………………………………….
v.      Nipimie unga kilo tano………………………………………………………………..
C. Sahihisha makosa katika sentensi zifuatazo kwa kuziandika kwa usahihi. (alama 05)
i.                    Ninachukua nafasi hii kuwashukuru
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
ii.                  Weka sahihi yako hapa.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
iii.                Sikuwa najua kuwa mwalimu wa Kiswahili anaitwa Mshiu.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
iv.                Katika ajali hiyo watu kumi waliuwawa.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..
v.                  Ninakwenda kesho kwa mjomba.
Kosa: ……………………………………………………………………..
Sahihi: ……………………………………………………………………..

SEHEMU C. (ALAMA 15)
SARUFI
3. A.  Eleza waziwazi kuhusu kazi za viambishi vilivyopigiwa mstari katika maneno yafuatayo.  (alama 06)
(a)    A-nacheza (kazi mbili)
(b)    Ana-vi-penda (kazi mbili)
(c)    Ruk-a (kazi moja)
(d)  Ana-ye-fundisha (kazi moja) 
B. Kupitia taaluma ya unyambulishaji badili majina/Nomino zifuatazo-kuwa vielezi (alama 03)
i.        Nyumba ……………………………………………………………………............
ii.      Bustani …………………………………………………………………….............
iii.    Hewa ……………………………………………………………………................
iv.    Daraja ……………………………………………………………………...............
v.      Kitanda . …………………………………………………………………….............
vi.    Uwanja  ………………………………………………………………………………..
C.  Chunguza jedwali lifuatalo kwa makini kasha jaza sehemu zilizoachwa wazi. ( alama06)
Neno
Mzizi
Kauli ya Kutendana
Kauli ya Kutendwa
Kusema
………………
Kuomba
………………
……………….
……………. ……………. …………….
-andik-
…………….
…………………..
Kupigana
Kuombana
…………………..
Kuimbana
Kusemwa
…………………….
…………………….
Kuandikwa
……………. ………

SEHEMU D. (ALAMA 40)
FASIHI SIMULIZI
4. A. Kazi za fasihi simulizi zina umuhimu gani kwa jamii? (alama 10)
   B. Kamilisha methali zifuatazo. (alama 10)
i.        ………………………………………..…………… yasiyo na ncha.
ii.      Usidharau dafu …………………………….……………………….
iii.    …………………………………….…………si mwisho wa uhunzi.
iv.    ………………………………………………………… i maji.
v.      Mtumi wa kunga ……………………………..…………………
D. Eleza kwa ufupi maana ya dhana zifuatazo kwa kutumia mifano halisi. (alama 20)
        i. Ubeti
       ii. Kipande
       iii. Mizan
       iv.    Urari
        v.      Vina

SEHEMU E. ( ALAMA 15)
UANDISHI WA INSHA/UTUNGAJI
5. A. Mtumie simu ya maandishi baba yako aitwaye Michael Martin wa Sanduku la Posta 333 Moshi, ukiweleza kuhusu mdogo wako aitwaye Maringo Michael aliyevunjika mguu wakati akicheza mpira wa miguu katika mashindano ya UMISETA yaliyofanyika katika uwanja wa Shule ya Bwiru Wavulana. Jina lako ni Shukuru Michael. (simu yako iwe na maneno kumi tu )   (alama 05).

B. Chora kielelezo cha muundo wa Barua Rasmi. (alama 10)




------------------------------- MWISHO ------------------------------------
Jua na Mwezi Havifanyi Kazi kwa Pamoja Japo Vyote Hutoa Mwanga.
*******************************************************************************************
 † † † † †  MR. MSHIU S.E  † † † † †

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni